eng1

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba Zanzibar, Bi Mwanaisha Alli Said ameendeleza ziara yake kisiwani Pemba na kupata nafasi ya kukutana na Afisa Mdhamin wa Wizara ya Maji, Nishati na Madini Muhandisi. Suleiman Hamad Omar ambae kabla ya nafasi yake hio, alikua Mkurugenzi wa Ofisi ya Shirika la Nyumba Pemba. Pamoja, walibadilishana mawazo na kujadili mambo mbali mbali ya maendeleo  yanayohusiana na Shirika la Nyumba kwa upande wa Pemba. 

Vilevile, Bi. Mwanaisha alifanya ziara ya ukaguzi wa nyumba za Maendeleo za Micheweni na Nyumba za Vijiji za Maziwang'ombe kwa kufanya mazungumzo na wapangaji aliowakuta na kuwashajihisha kulipa kodi kwa wakati ili Shirika liweze kuzifanyia matengenezo nyumba hizo pamoja na kuzitunza ili ziweze kuwafaa zaidi.
 
Wakati huo huo, Mkurugenzi alifanya ziara kwenye nyumba za Maendeleo zilizopo Wete na kukutana na Sheha wa Shehia ya Mtemani Bw.  Mrisho Juma Mtwana na kufanya nae mazungumzo kuhusu nyumba hizo  na kuomba mashirikiano yake kwenye masuala yote yanayohusu nyumba za Shirika zilizopo kwenye Shehia yake.
 
Pia  alikutana na wafanyakazi wa Ofisi ya Shirika la Nyumba ya Wete na kufanya nao kikao cha kujadili mambo mbali mbali juu ya majukumu yao na kuskiliza changamoto zinazowakabili. Mkurugenzi aliwasihi wafanyakazi hao kushirikiana vizuri na wafanyakazi wenzao wa Chakechake ili wazidi kuleta maendeleo kwenye Shirika. Aliwataka waje na mikakati mipya ya kukusanya kodi na kuongeza pato ili Shirika liweze kufanya kazi zake kwa vizuri na kufanikisha malengo yake.

eng3

 

News and Events

Ziara katika Ujenzi wa Nyumba Makaazi na Biashara Mombasa

Ziara katika Ujenzi wa Nyumba Makaazi na Biashara Mombasa

Mkurugenzi Mkuu Shirika la Nyumba Zanzibar ( wa nne kushoto) ndg. Mwanaisha Ali Said akiwa katika ziara ya Waziri Ardhi...

Menejimenti ya Shirika la Nyumba na Kamati ya Baraza la Wawakilishi

Menejimenti ya Shirika la Nyumba na Kamati ya Baraza la Wawakilishi

Menejimenti ya Shirika la Nyumba wakiwa kwenye Kikao cha Kamati ya Baraza la Wawakilishi ya kuchunguza na kudhibiti hesabu za...

Ziara ya Kamati ya Mawasiliano, Ardhi na Nishati ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar katika Nyumba za Maendeleo Michenzani.

Ziara ya Kamati ya Mawasiliano, Ardhi na Nishati ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar katika Nyumba za Maendeleo Michenzani.

Katika kutekeleza majukumu yake, Kamati ya Mawasiliano, Ardhi na Nishati ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar imeambatana na Waziri wa Ardhi...

Ziara ya Viongozi wa ZHC na Wabunge kutoka Nchi ya Ujerumani.

Ziara ya Viongozi wa ZHC na Wabunge kutoka Nchi ya Ujerumani.

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba Zanzibar, Bi. Mwanaisha Alli Said na menejimenti ya Shirika wameambatana na Wabunge kutoka Nchi...

Ziara ya Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar kukagua mradi wa matengenezo ya Nyumba namba 1699/1705 - Mnadani

Ziara ya Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar kukagua mradi wa matengenezo ya Nyumba namba 1699/1705 - Mnadani

Makamu wa pili wa Rais wa Zanzibar, Mhe. Hemed Suleiman Abdulla, amefanya ziara ya kukagua mradi wa matengenezo ya Nyumba...

Mkutano wa Wadau kujadili fursa za Ujenzi wa Nyumba za bei nafuu Zanzibar

Mkutano wa Wadau kujadili fursa za Ujenzi wa Nyumba za bei nafuu Zanzibar

Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makaazi Zanzibar na Shelter Afrique kwa kushirikiana na Shirika la Nyumba Zanzibar imefanya mkutano...

Mode of Payment


All paymets received done by Control number

Paymet received though

PBZ Bank / PBZ Agent

TigoPesa / EzyPesa

Visit any ZHC Office for your Control number

Pemba Office


Mtaa wa Masingini

Barabara Kuu

P. O. BOX 349

Chake Chake Pemba

Email: zhcpba@zhc.go.tz

Zanzibar Head Office


Zanzibar Housing Corporation

Sonara Building, Darajani

Creek Road

P. O. BOX 795

E-mail: This email address is being protected from spambots. You need JavaScript enabled to view it.

71124 Zanzibar..