pl2

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba Zanzibar, Bi. Mwanaisha Alli Said, alifanya ziara ya ukaguzi wa maeneo ya uwekezaji ya Shirika yaliyopo Chakechake pamoja na Maduka ya biashara na kufanya mazungumzo na baadhi ya Wapangaji wa maduka hayo ambapo aliwashajihisha kulipa kodi kwa wakati na kufuata masharti ya mikataba yao kwani kutokufanya hivyo kutapelekea  Shirika kuchukua hatua za Kisheria juu yao.

Aidha, alitembelea kwenye Nyumba za Vijiji za Kengeja na Mwambe pamoja na Nyumba za Maendeleo za Mapinduzi zilizopo Mkoani ambapo alipata nafasi ya kuongea na Diwani Mhe. Mrisho Juma Mtwana na kumuomba ushirikiano wake kwenye masuala yote yanayohusiana na Nyumba za Shirika zilizopo katika Wadi yake.
 
Alimalizia ziara yake kwa kufanya kikao na wapangaji wa nyumba za Madungu na Machomane kwa ajili ya kujitambulisha kwao na kuwashajihisha kulipa kodi kwa wakati ili Shirika liweze kumalizia  na matengenezo ya nyumba za Madungu na kuweza kufanya matengenezo kwenye nyumba nyengine zaid pamoja na kujenga nyumba kwa ajili ya kuwapatia Wazanzibari wengine makaazi bora. Na aliwasihi wapangaji hao kufuata Sheria na kuacha tabia za kukodisha au kutoa vilemba nyumba za Shirika na atakaejulikana anafanya hivyo hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yake.

pl2

 

Pay to PBZ Bank


All paymets received done by Control number

Visit any ZHC Office for your Control number

Pemba Office


ZHC Branch Miembeni Chake Chake Pemba

P. O. BOX 128

Email: zhcpba@zhc.go.tz

Pemba.

Zanzibar Head Office


Zanzibar Housing Corporation

Darajani Opposite to Petrol Station

Zanzibar

P. O. BOX 795

E-mail: This email address is being protected from spambots. You need JavaScript enabled to view it.

Zanzibar - Tanzania