wchakeMkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba Zanzibar, Bi.Mwanaisha Alli Said, amefanya ziara ya kikazi Pemba kwa kutembelea Ofisi kuu ya Shirika la Nyumba iliopo mjini Chakechake.

Katika ziara hio amekutana na Watendaji wakuu na wafanyakazi wa Ofisi hio kwa lengo la kujitambulisha na kuzungumzia mikakati ya utekelezaji kazi ya Shirika kwa upande wa Pemba na changamoto zinazolikabili Shirika. Vilevile amejadili hatua mbali mbali za kutatua changamoto hizo ili kuboresha utendaji kazi, ili Shirika liweze kupiga hatua zaidi.

Vile vile, Mkurugenzi alifanya majadiliano juu ya majukumu ya wafanyakazi hao na kusikiliza changamoto zinazowakabili. Pia aliwasihi wafanyakazi hao kufanya kazi kwa weledi, uaminifu na kushirikiana nae kwenye kuleta maendeleo kwenye Shirika kwa kupunguza matumizi yasiyo ya lazima. Pia, aliwasihi wafanyakazi hao kubuni mbinu mpya za kuwahamasisha wapangaji kulipa kodi kwa wakati ili Shirika lipate pato zaidi la kuweka kwenye Uwekezaji wa ujenzi wa nyumba nyingi zaid ili liweze kuwapatia wananchi makaazi bora pamoja na kuzifanyia ukarabati nyumba zilizopo chini ya Shirika.

Wakati huo huo Bi. Mwanaisha alifanya ziara kwenye Nyumba mbalimbali za Shirika zikiwemo Nyumba za Maendeleo za Madungu, Nyumba za Maendeleo za Machomane, Jaani Building, pamoja na kwenda kuona ujenzi wa Septic Tank (Karo) iliopo Tibirinzi.

karo1

News and Events

Ziara katika Ujenzi wa Nyumba Makaazi na Biashara Mombasa

Ziara katika Ujenzi wa Nyumba Makaazi na Biashara Mombasa

Mkurugenzi Mkuu Shirika la Nyumba Zanzibar ( wa nne kushoto) ndg. Mwanaisha Ali Said akiwa katika ziara ya Waziri Ardhi...

Menejimenti ya Shirika la Nyumba na Kamati ya Baraza la Wawakilishi

Menejimenti ya Shirika la Nyumba na Kamati ya Baraza la Wawakilishi

Menejimenti ya Shirika la Nyumba wakiwa kwenye Kikao cha Kamati ya Baraza la Wawakilishi ya kuchunguza na kudhibiti hesabu za...

Ziara ya Kamati ya Mawasiliano, Ardhi na Nishati ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar katika Nyumba za Maendeleo Michenzani.

Ziara ya Kamati ya Mawasiliano, Ardhi na Nishati ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar katika Nyumba za Maendeleo Michenzani.

Katika kutekeleza majukumu yake, Kamati ya Mawasiliano, Ardhi na Nishati ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar imeambatana na Waziri wa Ardhi...

Ziara ya Viongozi wa ZHC na Wabunge kutoka Nchi ya Ujerumani.

Ziara ya Viongozi wa ZHC na Wabunge kutoka Nchi ya Ujerumani.

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba Zanzibar, Bi. Mwanaisha Alli Said na menejimenti ya Shirika wameambatana na Wabunge kutoka Nchi...

Ziara ya Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar kukagua mradi wa matengenezo ya Nyumba namba 1699/1705 - Mnadani

Ziara ya Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar kukagua mradi wa matengenezo ya Nyumba namba 1699/1705 - Mnadani

Makamu wa pili wa Rais wa Zanzibar, Mhe. Hemed Suleiman Abdulla, amefanya ziara ya kukagua mradi wa matengenezo ya Nyumba...

Mkutano wa Wadau kujadili fursa za Ujenzi wa Nyumba za bei nafuu Zanzibar

Mkutano wa Wadau kujadili fursa za Ujenzi wa Nyumba za bei nafuu Zanzibar

Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makaazi Zanzibar na Shelter Afrique kwa kushirikiana na Shirika la Nyumba Zanzibar imefanya mkutano...

Mode of Payment


All paymets received done by Control number

Paymet received though

PBZ Bank / PBZ Agent

TigoPesa / EzyPesa

Visit any ZHC Office for your Control number

Pemba Office


Mtaa wa Masingini

Barabara Kuu

P. O. BOX 349

Chake Chake Pemba

Email: zhcpba@zhc.go.tz

Zanzibar Head Office


Zanzibar Housing Corporation

Sonara Building, Darajani

Creek Road

P. O. BOX 795

E-mail: This email address is being protected from spambots. You need JavaScript enabled to view it.

71124 Zanzibar..