Mkurugenzi Mkuu wa Shirika alifanya majadiliano na waandishi wa habari kuhusu wapangaji wa Jumba la mnadani. Ambapo aliwaelewa juu ya wapangaji hao kugoma kuhama kwenye Nyumba hio ili kupisha matengenezo ya nyumba hio ingali kuwa wamepewa mda wa kutosha kuweza kujipanga kuhama na kupewa notisi ya mwisho ya kutakiwa kuhama ifikapo saa nane ya tarehe 11/06/2021. Baada ya wapangaji kukiuka agizo hilo Viongozi na wafanyakazi wa Shirika kwa kushirikiana na Mkuu wa Wilaya Mhe. Rashid Simai Msaraka walifanikiwa kwenda eneo la tukio na kuwahamisha wapangaji hao na hata kuwapa msaada wa usafiri wa kuhamisha vitu vyao. Nyumba hio imekabidhiwa rasmi leo kwa Mkandarasi Yasin and Sons tayari kwa kuanza matengenzo hayo.